22. Mwenendo wa Kikristo
Tumeitwa kuwa watauwa wanaofikiri, kujisikia, na kutenda kulingana na kanuni za mbinguni. Ili Roho aumbe upya ndani yetu tabia ya Bwana wetu tunajihusisha tu katika mambo yale ambayo yatazaa katika maisha yetu usafi unaofanana na Kristo, afya na furaha katika maisha yetu. Hii inamaanisha kwamba maraha na maburudisho yetu yanapaswa kufikia viwango vikuu vya maonji na uzuri wa Kikristo. Huku tukitambua tofauti za kiutamaduni, mavazi yetu yanapaswa yawe ya kawaida, si ya anasa; na safi, yanayostahili wale ambao uzuri wao wa kweli asili yake siyo mapambo ya nje, bali asili yake ni mapambo yasiyoharibika, yenye roho ya upole na utulivu. Pia inamaanisha kwamba kwa kuwa miili yetu ni mahekalu ya Roho Mtakatifu, tunapaswa kuitunza kwa akili yenye afya sana kadiri invyowezekana na kuepuka vyakula vilivyo najisi, vilivyotajwa katika Maandiko Matakatifu. Kwa vile vinywaji vya vileo, tumbaku na maatumizi mabaya ya madawa hudhuru miili yetu, yatupasa kuepukana navyo pia. Badala yake tunapaswa kujishughulisha na cho chote kile kitakacholeta mawazo yetu na miili yetu viwe katika nidhamu ya Kristo, ambaye hutamani uzima wetu, furaha na wema
Mafungu ya Biblia
Warumi 12:1, 2; IYoh. 7; 2:6; Waef. 5:1 – 21; Wafilipi 4:8; IIWakor. 10:5; 6:14 – 7:1; IPet. 3:1 – 4; IWakor. 6:19, 20; 10:31; Walawi 11:1 – 47; IIIYoh. 2
